Wakazi wa kijiji cha Utambalila kilichopo kwenye wilaya ya Mbozi mkoani Songwe ambao walikumbwa na maafa ya kuharibikiwa kwa makazi yao sambamba na mashamba kufuatia mvua ya mawe iliyonyesha mapema wiki hii wamepatiwa msaada wa mbao za kujengea makazi yao sambamba na mbegu za mahindi kwa ajili ya kilimo.